Friday 19 December 2014


Pichani ni Bosi wa IPTL Bwana  Harbinder Singh Sethi
NA KAROLI VINSENT
RAIS  Jakaya Kikwete amehailisha Mkutano wake kati ya Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam  uliokuwa ufanyike leo Katika Ukumbi wa Ubungo plaza mpaka Jumatatu ya Wiki Ijayo.
    Sababu ya Kuhailisha Mkutano huo bado haijasemwa ila Wadadisi wa masuala ya Mambo wanasema Sababu ya Rais Jakaya Kikwete Kuhailisha Mkutano huo inatokana na  Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) na wenzake wawili, kufungua kesi ya kikatiba katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wakiiomba  itoe amri ya kuzuia utekelezaji wa maazimio nane ya Bunge kuhusu kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh bilioni 300 katika akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).



 Mbali na hao,Wengine waliofungua kesi hiyo namba 59 ya mwaka 2014, ni kampuni ya Pan Power Solution Tanzania (PAP) na mmiliki wake, Harbinder Singh Sethi.IPTL, PAP na Sethi walifungua kesi hiyo jana chini ya hati ya dharura kupitia kampuni za mawakili ya Bulwark, Asyla na Marando and Mnyele.

          Wadaiwa katika kesi hiyo ni Waziri Mkuu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), Spika wa Bunge na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

               Katika hati ya madai iliyowasilishwa katika mahakama hiyo jana, wadai wanapinga maazimio ya Bunge kutekelezwa wakidai kwamba, kilichofanyika bungeni ni kinyume cha katiba ya nchi.

           Wanadai maazimio hayo yanalenga kugombanisha mihimili mitatu ya dola na kwamba, yaliegemea upande mmoja.Pia wanadai kwamba, kuna kesi mbalimbali zinazoendelea mahakamani zinazohusiana na sakata la fedha hizo.

           Vilevile, wanadai Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alifanya ukaguzi, pia Takukuru ilifanya uchunguzi, hatimaye taarifa ya CAG ikajadiliwa bungeni.
 Wanadai kwamba mjadala huo ulisababisha Bunge kufikia maazimio hayo.

          Wadai hao wanadai kitendo hicho kilipuuza amri ya Mahakama Kuu kwa kufuata tafsiri potofu iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria kuhusu amri iliyozuia mjadala wa akaunti hiyo kufanyika bungeni.

          Kutokana na sababu hizo, wanaiomba mahakama izuie utekelezwaji wa maazimio ya Bunge.Pia itangaze maazimio hayo yaliyofikiwa Novemba 29, mwaka huu na maamuzi ya Spika wa Bunge kuyakubali, kuwa ni kinyume cha katiba ya nchi.

        Kesi hiyo iliyofunguliwa leo mchana, inatarajiwa kuanza kusikilizwa mara tu baada ya jopo la majaji watakapoteuliwa.

MAAZIMIO YA BUNGE
Azimio la kwanza lililofikiwa na Bunge linataka Takukuru, Jeshi la Polisi na vyombo vingine husika vya ulinzi na usalama kuwachukulia hatua stahiki za kisheria watu wote waliotajwa na taarifa maalumu ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (CAG) kuhusika na kashfa hiyo na watu wengine watakaogundulika kuhusika kufuatia uchunguzi mbali mbali unaoendelea.

La pili linataka Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhingo; Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka; aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema; Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi na wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wawajibishwe, kwa kuishauri mamlaka yao ya uteuzi kutengua uteuzi wao.

Wengine waliotajwa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusika katika kashfa hiyo ni Sethi na mmiliki wa kampuni ya VIP Engineering and Marketing, James Rugemalira.

Azimio la tatu linataka kamati za kudumu za Bunge zichukue hatua za haraka kabla ya mkutano wa 18 wa Bunge, kuwavua nyadhifa wenyeviti wa kamati za Bunge; Andrew Chenge (Bajeti), Victor Mwambalaswa (Nishati na Madini) na William Ngeleja (Katiba, Sheria na Utawala).

La nne linataka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuunda Tume ya Kijaji ya Uchunguzi kuchunguza tuhuma za utovu wa maadili dhidi ya Jaji Aloysius Mujulizi na Jaji Profesa Eudes Ruhangisa wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Azimio la tano linataka mamlaka husika za kifedha na za kiuchunguzi kuitaja Benki ya Stanbic Bank (Tanzania) Ltd na benki nyingine yoyote itakayogundulika kufuatia uchunguzi wa mamlaka za kiuchunguzi, kujihusisha na utakatishaji wa fedha zilizotolewa katika akaunti hiyo, kuwa ni taasisi zenye shaka ya utakatishaji wa fedha haramu.

 La sita linataka serikali iandae na kuwasilisha muswada wa marekebisho ya sheria iliyoiunda Takukuru kwa lengo la kuanzisha taasisi mahsusi itakayoshughulikia, kupambana na kudhibiti vitendo vya rushwa kubwa, ufisadi na hujuma za uchumi zinazotishia uhai wa taifa kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Azimio la saba linataka serikali iangalie uwezekano wa kununua mitambo ya kufua umeme ya IPTL na kuimilikisha kwa Tanesco kwa lengo la kuokoa fedha za shirika hilo.

Na azimio la nane linataka serikali itekeleze azimio husika la Bunge mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile kabla ya kumalizika kwa Mkutano wa Bunge la Bajeti na serikali iwasilishe taarifa ya utekelezaji wa mapitio ya mikataba ya umeme.

Stori:waandishi wetu

MENGINE yameibuka! Kifo cha aliyekuwa mnenguaji wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’, Mwanaisha Mohamed Mbegu ‘Aisha Madinda’ kimeibua mengine ambapo baadhi ya watu wa karibu wanaamini kimetokana na kudungwa sindano tano za majimaji yenye madawa ya kulevya, ‘unga’ na rafiki yake, Ijumaa ‘Kubwa’ linakupa zaidi.
Marehemu Mwanaisha Mohamed Mbegu ‘Aisha Madinda’enzi za uhai wake.
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Aisha alidungwa kwa makusudi sindano hizo na rafiki yake mmoja ambaye polisi bado wanamtafuta, ikidaiwa lengo lilikuwa kummaliza.
YALIYOSEMWA
Akizungumza kwenye msiba wa mnenguaji huyo nyota nyumbani kulikokuwa na kilio, Kigamboni jijini Dar, mwombolezaji mmoja ambaye ni mtu wa karibu na marehemu alisema:
“Unajua siku za karibuni, Aisha alirudia kubwia unga kama zamani, sasa majuzi mimi nilikutana naye akasema yuko kwa rafiki yake, Mwananyamala (Dar), lakini huyo rafiki aliyenitajia ni mmbwia unga mkubwa na amekuwa akiwadunga sindano wenzake.

Mtoto wa marehemu Aisha, Naomi akiwa katika majonzi.
“Sasa si unajua kwamba, sindano zile ukidungwa bila kipimo ni sumu mwilini. Uwezekano ni mkubwa kwamba, sindano alizodungwa na mwenzake ndizo zimechukua uhai wake,” kilidai chanzo hicho.
CHANZO KINGINE
Kwa mujibu wa chanzo kingine msibani hapo, upo wasiwasi kwamba tangu Aisha arejee Bongo akitokea Dubai kuna mtu amekuwa akimtishia maisha kwamba atamtoa roho.
Chanzo hicho kilidai kwamba, staa huyo ambaye alirudi akiwa vizuri amekuwa akipewa vitisho na mtu huyo bila kutaja sababu.
SIKU YA KIFO
Siku ya tukio, juzi Jumatano, habari zinadai kwamba, Mkurugenzi wa Vipindi wa Radio Clouds FM, Ruge Mutahaba alipigiwa simu na daktari mmoja wa Hospitali ya Mkoa wa Kitabibu Kinondoni, Mwananyamala na kuambiwa kuwa, kuna mwili wa mtu anayefanana na Aisha Madinda umetelekezwa hospitalini hapo na watu wasiojulikana na wameondoka.
Baada ya taarifa hizo, Ruge alimwendea hewani Bosi wa Bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka na kumjulisha madai ya daktari.
“Asha Baraka alikuwa Kigoma. Kwa hiyo alipopewa taarifa hizo alimpigia simu kiongozi wa wanamuziki wa Twanga Pepeta, Luiza Nyoni Mbutu na kumpa maelekezo kwamba afuatilie habari alizoambiwa na Ruge kama ni kweli.”
Mkurugenzi wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’Asha Baraka.
AISHA MADINDA NDANI YA MOCHWARI
Ikazidi kudaiwa kuwa, Luiza na wanamuziki wenzake, Lilian Tungaraza ‘Lilian Intaneti’ na Maria Soloma walifunga safari hadi Mwananyamala na kuukuta mwili wa Aisha ukiwa tayari mochwari, wakamjulisha Asha ambaye  alifunga safari na machozi juu kurejea Dar.
MTOTO WA MAREHEMU, ANAITWA NAOMI
Akizungumza na gazeti hili ndani ya Hospitali ya Mwananyamala muda mfupi baada ya mwili wa mama yake kuingizwa mochwari, binti wa Aisha, Naomi  huku akimwaga machozi, alisema:
“Mama alikuwa akiishi Kigamboni siku za karibuni. Mimi pia nikaamua kwenda kuishi naye.”
Akaendelea: “Kuna kama siku tatu nyuma mama hakuwa akilala nyumbani, jana (Jumanne sasa), asubuhi mama alinitumia meseji akisema anaomba nimtumie pesa, nikamtumia.
“Lakini leo (juzi, Jumatano) mchanamchana nilisema nimpigie simu mama nimuulize huko aliko anaendeleaje? Kabla sijafanya hivyo, mama mkubwa alinitumia meseji na kuniambia mama amefariki dunia, ndiyo nikaja huku.”
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere 'Steve Nyerere'(kulia) na Luiza Mbutu (katikati) wakihesabu michango iliyopokelewa kwa njia ya simu katika Hospitali ya Mwanayamala jijini Dar es Salaam. Kushoto ni mnenguaji wa kitambo, Lilian Intanet.
KIKAO CHA FAMILIA AELEZEA KIFO CHAKE!
Binti huyo aliendelea kusema kuwa, siku za karibu, marehemu aliwahi kuwaita ndugu zake na kuwapa ujumbe wa ajabu.
“Kuna siku aliwaita ndugu zake nyumbani akasema katika familia yetu wote, mimi ndiyo nitakayeanza kufa. Sijui mama alijua atakufa ndiyo maana akasema vile,” alisema binti huyo.
MASWALI YA MSINGI
Mpaka sasa maswali ambayo yalitawala msibani ni haya! Je, ni nani aliyeufikisha mwili wa marehemu Hospitali ya Mwananyamala na kuutelekeza? Je, dokta alijuaje kuwa alikuwa Aisha Madinda?
Je, mwili wake ulipelekwa hospitalini hapo na mtu mmoja au wengi? Walitumia usafiri gani? Bajaj au teksi? Ni vyema pia polisi wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar wakafuatilia kifo hiki kwa undani.

Thursday 18 December 2014


Wanasema ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni. Katika hali isiyo ya kawaida, mchumba wa zamani wa mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, Faiza Ally, amesherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kuvaa diapers!!



Sherehe hiyo ilifanyika juzi kwenye hoteli ya Seacliff na kuhudhuriwa na wageni kibao. Jionee mwenyewe picha zake!!








Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
Waziri Mizengo Pinda amekatiza kwa muda, ziara yake katika Falme za Kiarabu kwa maelezo kwamba ameitwa nyumbani na Rais Jakaya Kikwete kwa shughuli maalumu.
Waziri Mkuu ambaye yuko katika ziara ya kutembelea nchi za Falme za Kiarabu, ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano na kutafuta wawekezaji, amekatisha ziara hiyo siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kujiuzulu kutokana na kashfa ya Escrow.
Werema alijiuzulu juzi na Rais Kikwete akaridhia hatua hiyo, huku umma ukisubiri hatua zaidi dhidi ya mawaziri na watendaji wa Serikali waliotajwa katika sakata hilo.
Katika barua yake ya kujiuzulu, Jaji Werema alisema ushauri wake wa kisheria kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka na hivyo kuchafua hali ya hewa.
Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, leo Waziri Mkuu alitarajiwa kufanya mazungumzo na washiriki wa maonyesho ya B2B pamoja na kutembelea maeneo mengine lakini ziara hiyo imefutwa na badala yake anaondoka asubuhi kurudi nyumbani.
Baadaye leo Pinda alitakiwa kwenda Doha, Qatar kwa ziara kama hiyo hadi Desemba 23.
Baada ya kukamilisha jukumu aliloitiwa, Waziri Mkuu anatarajiwa kurejea Falme za Kiarabu Jumamosi kuendelea na ziara yake.
MWILI WA AISHA MADINDA KUPASULIWA ILI UCHUNGUZWE, SASA KUZIKWA KESHO IJUMAA


Aisha Madinda - enzi za uhai wake alipokuwa stejini.

ALIYEKUWA mnenguaji na mwimbaji wa Bendi ya Twanga Pepeta, Aisha Madinda aliyefariki jana asubuhi, atazikwa kesho mchana badala ya leo kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.

Mtoto wa kwanza marehemu, Feisal amesema kuwa polisi wamesema ni lazima mwili wa mama yake ufanyiwe upasuaji (postmortem) ili kujua chanzo cha kifo chake.

Awali ndugu wa marehemu walisema hawahitaji Asha Madinda afanyiwe upasuaji, lakini baada ya polisi kutembelea eneo la tukio la kifo chake huko Mabibo, wamesema ni lazima upasuaji ufanyike.

Feisal amesema upasuaji unatarajiwa kufanyika leo mchana hali inayowalazimisha kubadili ratiba ya mazishi. Aisha Madinda sasa atazikwa kesho mchana baada ya sala ya Ijumaa.
Wanajeshi wa jehsi la Nigeria
Mhakama moja ya kijeshi nchini Nigeria imewahukumu kifo askari 54 kwa kukataa kupigana na kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Boko Haram.
Wanajeshi hao ambao walipatikana na kosa la uasi,walituhumiwa kukataa kuikomboa miji mitatu iliyokuwa imetekwa na Boko Haram mwezi Agosti.
Wakili wa wanajeshi hao 54 alisema kuwa watawauwa kwa kupigwa risasi huku wengine watano wakiachiliwa huru.
Wanajeshi wamelalamika kuwa hawapewi silaha na mabomu ya kutosha kupigana na Boko Harm.
Kundi hilo limekuwa likipigana tangu mwaka 2009 na linalenga kujenga nchi inayoongozwa na sheria za Kiislamu kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Zaidi ya watu 2000 wameuwawa katika mashambulizi yaliyolaumiwa kufanywa na kundi hilo kufikia sasa mwaka huu na maelfu zaidi ya watu wamelazimishwa kuhama makwao kutokana na vita vinavyoendelea.
Koti hiyo ya kijeshi ilianza mwezi Oktoba na ilifanywa kwa siri.Viongozi wa kijeshi hawakupatikana kuzungumzia swala hilo.
Wakili anayewawakilisha,Femi Falana,alisema kuwa wanajeshi hao wote walituhumiwa ''kupanga njama ya kuasi dhidi ya mamlaka ya kikosi cha Divisheni ya 7 cha jeshi ya Nigeria.''
Wanajeshi wote walikataa mashtaka na hukumu hiyo inasubiri idhini ya maafisa wa ngazi za juu.
Katika kisa sawia mwezi Septemba,wanajeshi 12 walihukumiwa kifo kwa makosa ya uasi na jaribio la kumuua afisa wa jeshi katika mji wa kaskazini-mashariki wa Maiduguri.


Aisha Madinda akiwa na mkurugenzi wa ASET Asha Baraka.
Makala: Sifael Paul na Gladness Mallya
Amekwenda mapema mno! Siku ya Desemba 17, mwaka huu haikuwa poa hata kidogo kwenye tasnia ya muziki wa dansi Bongo katika kipengele cha unenguaji.
Chumba chetu cha habari cha Global Publishers kinachofanya kazi kwa karibu na mastaa Bongo kilipata mshtuko wa aina yake.
Zilikuwa ni habari mbaya za kifo cha aliyekuwa mnenguaji bei mbaya wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’ inayosimamiwa na Kampuni ya ASET chini ya mkurugenzi wake, Asha Baraka, Mwanaisha Mohamed Mbegu. Wengi tulimzoea kwa jina la stejini la Aisha Madinda.
AZALIWA OCEAN ROAD
Katika mahojiano aliyofanya na magazeti yetu kwa nyakati tofauti, kabla ya kujiingiza kwenye sanaa ya unenguaji na baada ya kuugua kwa muda mrefu kisha kupona na kukutwa na umauti, Aisha alieleza kwamba alizaliwa jijini Dar katika Hospitali ya Ocean Road.
KIGOMA
Hiyo ilikuwa Mei 5, 1979. Hivyo ameondoka mapema akiwa na umri wa miaka 35 tu. Baada ya maisha ya utoto, Aisha alipelekwa mkoani Kigoma ambako ndiko alikokulia.
Akiwa mkoani humo, Aisha alipata masomo yake ya msingi katika Shule ya Kiganamo iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma hadi alipohitimu darasa la saba mwaka 1992.
AISHIA FORM TWO
Mwaka 1993 alihamishia makazi yake mjini Kigoma na kujiunga na Sekondari ya Katubuka. Hata hivyo, Aisha hakufanikiwa kuhitimu masomo yake ya sekondari baada ya wazazi wake kushindwa kumlipia ada hivyo aliishia kidato cha pili (form two).
DAR
Mwaka 1994, Aisha alihamia jijini Dar na kuanza kazi ya usafi katika kampuni iliyojulikana kama Dar Cleaner. Alifanya kazi hiyo katika majengo mbalimbali ya jijini hivyo kufahamiana na watu wengi.
UNENGUAJI
Mwaka 1996 aliingia kwenye unenguaji baada ya prodyuza wa muziki aliyefahamika kwa jina moja la Maloni kumtonya kuwa Club Bilicanas ‘Bilz’ iliyopo Posta, Dar kulikuwa kunahitajika wanenguaji.
Akiwa Bilz, mwaka huohuo, klabu hiyo ilianzisha bendi iliyokwenda kwa jina la Bil Bams ndipo Aisha akaanza kuitumikia.
UARABUNI
Mwaka 1999, wakati huo, Aisha alishakuwa tishio katika kukata nyonga stejini huku akieleza jinsi alivyoipenda kazi yake hiyo.
Mwaka huohuo, alipata shavu la kwenda kupiga kazi Uarabuni katika Mji wa Muscat akiwa ameambatana na mcheza shoo mwenzake, Halima White ambaye sasa ni marehemu.
Walikaa nchini humo kwa takriban mwaka mmoja, mwaka 2000 walirejea Bongo wakiwa mambo safi.
BORABORA SOUND
Mwaka huo Aisha alijiunga na Bendi ya Borabora Sound ambayo aliitumikia kwa miezi sita kabla ya kusafiri tena kwenda Bahrain, Uarabuni kwa kazi hiyo ya unenguaji.
KILIMANJARO CONNECTION
Baadaye Aisha alirejea Dar kwa mara nyingine. Alijiunga na Bendi ya Kilimanjaro Connection ya jijini Dar ambapo pia hakukaa sana.
Mwaka 2000 mwishoni, aliachana na bendi hiyo kisha akawa anafanya biashara zake ndogondogo.
Aisha Madinda.
TWANGA PEPETA
Mwaka 2001, mkali huyo wa kukata nyonga anayeshikilia rekodi hiyo kwa kipindi chote alijiunga na Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’.
UHOLANZI
Aisha alifanya safari nyingi za kisanaa barani Ulaya akiwa na Twanga Pepeta lakini hawezi kusahau shoo aliyokwenda kufanya nchini Uholanzi katika Mji wa Amsterdam ambako alipokelewa kwa shangwe ya ajabu kiasi kwamba hakuamini macho yake.
EXTRA BONGO
Hapo alipiga kazi ya unenguaji hadi mwaka 2011 mwishoni alipohamia Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo Staili’.
Kwa bahati mbaya, wakati huo Aisha tayari alikuwa ameshatopea kwenye matumizi ya madawa ya kulevya hadi kufikia hatua ya kushindwa kunengua akisumbuliwa na tatizo la kuvimba miguu. Hata hivyo, alitangaza kuacha kutumia madawa hayo japokuwa baadaye kuliibuka ‘rumansi’ kuwa bado alikuwa akitumia.
REJEA TWANGA
Mwaka jana, mwanamama huyo alirejea Twanga Pepeta lakini bado alikuwa akisumbuliwa na miguu huku akitumia dozi ya kuacha madawa ya kulevya na kuhamasisha vijana kuacha ulevi huo mbaya unaomaliza nguvu ya taifa ambayo ni vijana.
OKOKA
Katika kutafuta msaada wa kiroho, Aisha aliokoka akawa anasali katika Kanisa la Zoe lililopo Segerea jijini Dar akiyakabidhi maisha yake kwa Mwenyezi Mungu hadi alipokutwa na umauti.
DUBAI
Hata hivyo, miezi kadhaa mwaka huu, mwanadada huyo alitimkia Dubai kwa ajili ya dili la kunengua lakini alipofika huko alijikuta akitumikishwa kazi za ndani na wenyeji wake kiasi cha ubalozi wa Tanzania huko Dubai kuingilia kati na kumrejesha nyumbani.
Design by GG greggy| Blogger Theme by greggy - Premium Blogger Templates | NewBloggerThemes.com