Thursday 18 December 2014


Wanasema ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni. Katika hali isiyo ya kawaida, mchumba wa zamani wa mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, Faiza Ally, amesherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kuvaa diapers!!



Sherehe hiyo ilifanyika juzi kwenye hoteli ya Seacliff na kuhudhuriwa na wageni kibao. Jionee mwenyewe picha zake!!








Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
Waziri Mizengo Pinda amekatiza kwa muda, ziara yake katika Falme za Kiarabu kwa maelezo kwamba ameitwa nyumbani na Rais Jakaya Kikwete kwa shughuli maalumu.
Waziri Mkuu ambaye yuko katika ziara ya kutembelea nchi za Falme za Kiarabu, ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano na kutafuta wawekezaji, amekatisha ziara hiyo siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kujiuzulu kutokana na kashfa ya Escrow.
Werema alijiuzulu juzi na Rais Kikwete akaridhia hatua hiyo, huku umma ukisubiri hatua zaidi dhidi ya mawaziri na watendaji wa Serikali waliotajwa katika sakata hilo.
Katika barua yake ya kujiuzulu, Jaji Werema alisema ushauri wake wa kisheria kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka na hivyo kuchafua hali ya hewa.
Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, leo Waziri Mkuu alitarajiwa kufanya mazungumzo na washiriki wa maonyesho ya B2B pamoja na kutembelea maeneo mengine lakini ziara hiyo imefutwa na badala yake anaondoka asubuhi kurudi nyumbani.
Baadaye leo Pinda alitakiwa kwenda Doha, Qatar kwa ziara kama hiyo hadi Desemba 23.
Baada ya kukamilisha jukumu aliloitiwa, Waziri Mkuu anatarajiwa kurejea Falme za Kiarabu Jumamosi kuendelea na ziara yake.
MWILI WA AISHA MADINDA KUPASULIWA ILI UCHUNGUZWE, SASA KUZIKWA KESHO IJUMAA


Aisha Madinda - enzi za uhai wake alipokuwa stejini.

ALIYEKUWA mnenguaji na mwimbaji wa Bendi ya Twanga Pepeta, Aisha Madinda aliyefariki jana asubuhi, atazikwa kesho mchana badala ya leo kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.

Mtoto wa kwanza marehemu, Feisal amesema kuwa polisi wamesema ni lazima mwili wa mama yake ufanyiwe upasuaji (postmortem) ili kujua chanzo cha kifo chake.

Awali ndugu wa marehemu walisema hawahitaji Asha Madinda afanyiwe upasuaji, lakini baada ya polisi kutembelea eneo la tukio la kifo chake huko Mabibo, wamesema ni lazima upasuaji ufanyike.

Feisal amesema upasuaji unatarajiwa kufanyika leo mchana hali inayowalazimisha kubadili ratiba ya mazishi. Aisha Madinda sasa atazikwa kesho mchana baada ya sala ya Ijumaa.
Wanajeshi wa jehsi la Nigeria
Mhakama moja ya kijeshi nchini Nigeria imewahukumu kifo askari 54 kwa kukataa kupigana na kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Boko Haram.
Wanajeshi hao ambao walipatikana na kosa la uasi,walituhumiwa kukataa kuikomboa miji mitatu iliyokuwa imetekwa na Boko Haram mwezi Agosti.
Wakili wa wanajeshi hao 54 alisema kuwa watawauwa kwa kupigwa risasi huku wengine watano wakiachiliwa huru.
Wanajeshi wamelalamika kuwa hawapewi silaha na mabomu ya kutosha kupigana na Boko Harm.
Kundi hilo limekuwa likipigana tangu mwaka 2009 na linalenga kujenga nchi inayoongozwa na sheria za Kiislamu kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Zaidi ya watu 2000 wameuwawa katika mashambulizi yaliyolaumiwa kufanywa na kundi hilo kufikia sasa mwaka huu na maelfu zaidi ya watu wamelazimishwa kuhama makwao kutokana na vita vinavyoendelea.
Koti hiyo ya kijeshi ilianza mwezi Oktoba na ilifanywa kwa siri.Viongozi wa kijeshi hawakupatikana kuzungumzia swala hilo.
Wakili anayewawakilisha,Femi Falana,alisema kuwa wanajeshi hao wote walituhumiwa ''kupanga njama ya kuasi dhidi ya mamlaka ya kikosi cha Divisheni ya 7 cha jeshi ya Nigeria.''
Wanajeshi wote walikataa mashtaka na hukumu hiyo inasubiri idhini ya maafisa wa ngazi za juu.
Katika kisa sawia mwezi Septemba,wanajeshi 12 walihukumiwa kifo kwa makosa ya uasi na jaribio la kumuua afisa wa jeshi katika mji wa kaskazini-mashariki wa Maiduguri.


Aisha Madinda akiwa na mkurugenzi wa ASET Asha Baraka.
Makala: Sifael Paul na Gladness Mallya
Amekwenda mapema mno! Siku ya Desemba 17, mwaka huu haikuwa poa hata kidogo kwenye tasnia ya muziki wa dansi Bongo katika kipengele cha unenguaji.
Chumba chetu cha habari cha Global Publishers kinachofanya kazi kwa karibu na mastaa Bongo kilipata mshtuko wa aina yake.
Zilikuwa ni habari mbaya za kifo cha aliyekuwa mnenguaji bei mbaya wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’ inayosimamiwa na Kampuni ya ASET chini ya mkurugenzi wake, Asha Baraka, Mwanaisha Mohamed Mbegu. Wengi tulimzoea kwa jina la stejini la Aisha Madinda.
AZALIWA OCEAN ROAD
Katika mahojiano aliyofanya na magazeti yetu kwa nyakati tofauti, kabla ya kujiingiza kwenye sanaa ya unenguaji na baada ya kuugua kwa muda mrefu kisha kupona na kukutwa na umauti, Aisha alieleza kwamba alizaliwa jijini Dar katika Hospitali ya Ocean Road.
KIGOMA
Hiyo ilikuwa Mei 5, 1979. Hivyo ameondoka mapema akiwa na umri wa miaka 35 tu. Baada ya maisha ya utoto, Aisha alipelekwa mkoani Kigoma ambako ndiko alikokulia.
Akiwa mkoani humo, Aisha alipata masomo yake ya msingi katika Shule ya Kiganamo iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma hadi alipohitimu darasa la saba mwaka 1992.
AISHIA FORM TWO
Mwaka 1993 alihamishia makazi yake mjini Kigoma na kujiunga na Sekondari ya Katubuka. Hata hivyo, Aisha hakufanikiwa kuhitimu masomo yake ya sekondari baada ya wazazi wake kushindwa kumlipia ada hivyo aliishia kidato cha pili (form two).
DAR
Mwaka 1994, Aisha alihamia jijini Dar na kuanza kazi ya usafi katika kampuni iliyojulikana kama Dar Cleaner. Alifanya kazi hiyo katika majengo mbalimbali ya jijini hivyo kufahamiana na watu wengi.
UNENGUAJI
Mwaka 1996 aliingia kwenye unenguaji baada ya prodyuza wa muziki aliyefahamika kwa jina moja la Maloni kumtonya kuwa Club Bilicanas ‘Bilz’ iliyopo Posta, Dar kulikuwa kunahitajika wanenguaji.
Akiwa Bilz, mwaka huohuo, klabu hiyo ilianzisha bendi iliyokwenda kwa jina la Bil Bams ndipo Aisha akaanza kuitumikia.
UARABUNI
Mwaka 1999, wakati huo, Aisha alishakuwa tishio katika kukata nyonga stejini huku akieleza jinsi alivyoipenda kazi yake hiyo.
Mwaka huohuo, alipata shavu la kwenda kupiga kazi Uarabuni katika Mji wa Muscat akiwa ameambatana na mcheza shoo mwenzake, Halima White ambaye sasa ni marehemu.
Walikaa nchini humo kwa takriban mwaka mmoja, mwaka 2000 walirejea Bongo wakiwa mambo safi.
BORABORA SOUND
Mwaka huo Aisha alijiunga na Bendi ya Borabora Sound ambayo aliitumikia kwa miezi sita kabla ya kusafiri tena kwenda Bahrain, Uarabuni kwa kazi hiyo ya unenguaji.
KILIMANJARO CONNECTION
Baadaye Aisha alirejea Dar kwa mara nyingine. Alijiunga na Bendi ya Kilimanjaro Connection ya jijini Dar ambapo pia hakukaa sana.
Mwaka 2000 mwishoni, aliachana na bendi hiyo kisha akawa anafanya biashara zake ndogondogo.
Aisha Madinda.
TWANGA PEPETA
Mwaka 2001, mkali huyo wa kukata nyonga anayeshikilia rekodi hiyo kwa kipindi chote alijiunga na Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’.
UHOLANZI
Aisha alifanya safari nyingi za kisanaa barani Ulaya akiwa na Twanga Pepeta lakini hawezi kusahau shoo aliyokwenda kufanya nchini Uholanzi katika Mji wa Amsterdam ambako alipokelewa kwa shangwe ya ajabu kiasi kwamba hakuamini macho yake.
EXTRA BONGO
Hapo alipiga kazi ya unenguaji hadi mwaka 2011 mwishoni alipohamia Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo Staili’.
Kwa bahati mbaya, wakati huo Aisha tayari alikuwa ameshatopea kwenye matumizi ya madawa ya kulevya hadi kufikia hatua ya kushindwa kunengua akisumbuliwa na tatizo la kuvimba miguu. Hata hivyo, alitangaza kuacha kutumia madawa hayo japokuwa baadaye kuliibuka ‘rumansi’ kuwa bado alikuwa akitumia.
REJEA TWANGA
Mwaka jana, mwanamama huyo alirejea Twanga Pepeta lakini bado alikuwa akisumbuliwa na miguu huku akitumia dozi ya kuacha madawa ya kulevya na kuhamasisha vijana kuacha ulevi huo mbaya unaomaliza nguvu ya taifa ambayo ni vijana.
OKOKA
Katika kutafuta msaada wa kiroho, Aisha aliokoka akawa anasali katika Kanisa la Zoe lililopo Segerea jijini Dar akiyakabidhi maisha yake kwa Mwenyezi Mungu hadi alipokutwa na umauti.
DUBAI
Hata hivyo, miezi kadhaa mwaka huu, mwanadada huyo alitimkia Dubai kwa ajili ya dili la kunengua lakini alipofika huko alijikuta akitumikishwa kazi za ndani na wenyeji wake kiasi cha ubalozi wa Tanzania huko Dubai kuingilia kati na kumrejesha nyumbani.


Wanasema ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni. Katika hali isiyo ya kawaida, mchumba wa zamani wa mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, Faiza Ally, amesherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kuvaa diapers!!



Sherehe hiyo ilifanyika juzi kwenye hoteli ya Seacliff na kuhudhuriwa na wageni kibao. Jionee mwenyewe picha zake!!










Design by GG greggy| Blogger Theme by greggy - Premium Blogger Templates | NewBloggerThemes.com