Sunday 2 November 2014

Jeshi laombwa kurudisha mamlaka kwa raia

  • Saa moja iliyopita

Marekani imelaani kile ilichokitaja kuwa mipango ya jeshi nchini Burkina Faso ya kulazimisha inachotaka kwa watu raia kufuatia kujiuzulu kwa rais wa nchi hiyo Blaise Compaore.
Jeshi limemteua kanali Isaac Zida kama kiongozi mpya wa serikali ya mpito.
Lakini kwa upande wake Marekani inataka kuwepo utawala wa kiraia nchini Burkina Faso mbali na mipango ya kuwepo kwa uchaguzi wa urais, wito ambao pia ulitolewa na muungano wa Afrika.
Kanali Issac Zida ambaye ameteuliwa na jeshi kuongoza serikali ya Mpito ya Burkina Faso.
Upinzani nchini Burkina Faso unasema kuwa hautakubali uongozi wa kijeshi na umeitisha maandamano leo Jumapili
Bwana Compaore ameikimbilia Ivory Coast baada ya kulazimishwa kuondoka madarakani kupitia maandamano.

0 comments:

Post a Comment

Design by GG greggy| Blogger Theme by greggy - Premium Blogger Templates | NewBloggerThemes.com