Wednesday 1 October 2014

Makubwa! Mwanadada asiyeishiwa matukio Bongo, Lulu Semagongo ‘Anti Lulu’ ameangusha bonge la pati huku ikihudhuriwa na mashoga kibao. 

Wanaume 'tata' wakilishana keki katika sherehe ya bethidei. 
 
Pati hiyo ya kufuru ambayo ilikuwa ni ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya kijana wa mjini aliyetajwa kwa jina moja la Abdul iliyoandaliwa na Anti Lulu ilifanyika katika Hoteli ya KB iliyopo Kijitonyama, Dar, wikiendi iliyopita ambapo ilihudhuriwa na watu mbalimbali lakini asilimia kubwa ya waalikwa walikuwa ni ‘wanaume tata’. 
 
Aunty Lulu akikata mauno kwa raha zake. 
 
Ijumaa Wikienda lilifanikiwa kuzama ndani ‘kimafia’ ambapo lilimshuhudia Anti Lulu akikata mauno ya kufa mtu baada ya kusikia kibao kata kilichokuwepo hotelini hapo. 
 
Wageni waalikwa wakiendelea kujiachia katika bethidei hiyo. 
 
Katika pati hiyo wanawake wengi walionekana wakiwa nusu utupu na wengine baada ya kuingia walivua nguo na kuvaa vichupi na braa kisha kuzama kwenye bwawa la kuogelea wakifuatiwa na mashoga hao waliokuwa wamevalia boksa na singlendi

0 comments:

Post a Comment

Design by GG greggy| Blogger Theme by greggy - Premium Blogger Templates | NewBloggerThemes.com